• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mkinga District Council
Mkinga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Livestock and Fishary
      • Works and Fire Recure
      • Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ugavi
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Legal
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma wa Maji
    • Huduma ya Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Maktaba ya Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Matukio
    • Habari
    • Matukio

WITO WATOLEWA KWA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA KWA AMANI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29,2025

Posted on: October 23rd, 2025

Na: Nassoro Rashid – Mkinga, Tanga

Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Mhe. Gilbert Kalima, ametoa wito kwa wananchi wa wilaya hiyo kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025, akisisitiza umuhimu wa kudumisha amani, mshikamano na utulivu katika kipindi chote cha uchaguzi.

Akizungumza katika kikao na viongozi wa dini wa Kiislamu na Kikristo, Mhe. Kalima alisema serikali inaendelea kutekeleza kalenda ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa mafanikio makubwa, huku hali ya utulivu ikiendelea kutamalaki katika Wilaya ya Mkinga.

“Tunaenda kuhitimisha kalenda ya Tume ya Uchaguzi kwa mafanikio makubwa. Ndani ya wilaya yetu amani na utulivu imetamalaki. Wapiga kura zaidi ya asilimia 80 wamejitokeza, jambo linaloonesha ushirikiano mkubwa kati ya serikali na viongozi wa dini,” alisema Mhe. Kalima.

Aidha, alibainisha kuwa kuanzia Oktoba 25, 2025, Tume itaanza kutoa matangazo rasmi katika maeneo yote ya wilaya ili kuwaelimisha na kuwakumbusha wananchi umuhimu wa kujitokeza kupiga kura.

“Tunaomba viongozi wa dini waendelee kutumia majukwaa ya ibada – Ijumaa, Jumamosi na Jumapili – kuwakumbusha waumini kwamba tarehe 29 ni siku muhimu ya uchaguzi. Wajitokeze kwa wingi bila hofu, kwani serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea,” aliongeza Mhe. Kalima.

Kwa upande wake, Kadhi wa Wilaya ya Mkinga, Sheikh Omari Zimbwe, alisema viongozi wa Kiislamu wamepokea kwa mikono miwili wito huo wa Mkuu wa Wilaya na wamepanga kuutumia mkutano wa Ijumaa kuhamasisha waumini kushiriki uchaguzi kwa amani.

“Sisi kama viongozi wa Kiislamu tumeupokea wito huu kwa moyo wa upendo, na tutaendelea kuwakumbusha waumini wetu wajitokeze kwa wingi siku ya uchaguzi. Tunawaomba waende kupiga kura kwa utulivu na kudumisha amani kama ilivyo desturi yetu katika Mkinga,” alisema Sheikh Zimbwe.

Naye Mchungaji Julius Clement Mtoi, Mwenyekiti wa Umoja wa Makanisa ya Kipentekoste Wilaya ya Mkinga, alisema viongozi wa Kikristo pia wameungana na serikali kuhimiza ushiriki wa wananchi katika uchaguzi kwa amani na upendo, wakitumia ibada za Jumamosi na Jumapili kama sehemu ya kuelimisha waumini.

“Tutaendelea kuhimiza waumini wetu kutumia haki yao ya kidemokrasia kwa amani na upendo. Jumamosi na Jumapili tutaendelea kuwakumbusha waumini wote wajitokeze kwa wingi kupiga kura na kudumisha utulivu kama ishara ya imani na umoja wetu,” alisema Mchungaji Mtoi.

Mhe. Kalima alihitimisha kikao hicho kwa kuwahakikishia wananchi wote kuwa serikali imejipanga vyema kuhakikisha zoezi la upigaji kura linafanyika katika mazingira ya amani, usalama na utulivu, huku akiwataka wananchi kuendelea na shughuli zao za maendeleo mara baada ya kumaliza kupiga kura.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA October 16, 2023
  • HATI MILIKI ZA ARDHI ZILIZOKAMILIKA WILAYA MKINGA December 04, 2022
  • KUSAFISHA MAENEO KWA WAMILIKI WA VIWANJA MKINGA August 12, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA July 18, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA CHAKULA DUNIANI KWA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA UZALISHAJI WA CHAKULA

    October 16, 2025
  • TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA CHAKULA DUNIANI KWA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA UZALISHAJI WA CHAKULA

    October 16, 2025
  • WITO WATOLEWA KWA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA KWA AMANI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29,2025

    October 23, 2025
  • MAKARANI WAOMNGOZAJI WAPIGA KURA WAASWA KUWA WAADILIFU

    October 25, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

Angalia zaidi

Kurasa za Haraka

  • Fomu za Maombi
  • Habari

Kurasa Mashuhuri

  • OR- TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Salary slip portal
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Taifa
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Kasera, Tanga -HorohoroRoad

    Postal Address: P O Box 6005 Tanga

    Simu: +255 027-2660501

    Simu: +255 684 625 299

    Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Huduma

Mkinga dc @ 2017