• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mkinga District Council
Mkinga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Livestock and Fishary
      • Works and Fire Recure
      • Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ugavi
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Legal
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma wa Maji
    • Huduma ya Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Maktaba ya Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Matukio
    • Habari
    • Matukio

ULIPAJI FIDIA MKOMAZI NI USHUHUDA WA SERIKALI SIKIVU

Posted on: December 4th, 2025

Na: Nassoro Rashid - Mkinga

Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Mhe. Gilbert Sylvester Kalima, amewashukuru wananchi wa Mkinga kwa ushirikiano mkubwa wanaouonesha katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Serikali, hususan zoezi la ulipaji fidia kwa wakazi wanaopisha Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi.

Mhe. Kalima alitoa kauli hiyo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Batilda Buriani, wakati wa hafla ya kukabidhi hundi za fidia kwa wananchi waliohamishwa kupisha hifadhi hiyo lililofanyika katika kijiji cha Mwakijembe Wilayani Mkinga.

Mkuu huyo wa Wilaya alitumia nafasi hiyo kufikisha salamu za shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuleta maendeleo ndani ya wilaya hiyo, ikiwemo kutoa fedha za fidia shilingi Milioni 700 kwa wananchi wanaohamishwa kupisha shughuli za Serikali. Alibainisha kuwa hatua hiyo ni uthibitisho wa serikali sikivu na inayowajali wananchi wake.

Akiyataja mafanikio ya karibuni, Mhe. Kalima alisema serikali tayari imetoa fidia kwa wakazi wa Mtimbwani na Kwale kutokana na maeneo yao kuchukuliwa kwa shughuli za maendeleo. Sambamba na hilo, aliweka wazi kuwa mchakato wa fidia kwa wananchi 28 waliotoa maeneo yao kwa ajili ya shughuli za usalama mpakani upo katika hatua za mwisho.

“Naomba wananchi wetu hawa 28 waendelee kuwa na subira. Wamevuta subira kwa muda mrefu, naomba waendelee kuvuta subira kwa sababu mchakato huu upo kwenye hatua za mwisho,” alisisitiza.

Aidha, aliwahakikishia wananchi waliopisha upanuzi wa barabara ya Tanga–Horohoro kuwa serikali inautazama kwa ukaribu mchakato wa ulipaji fidia zao na muda ukifika taratibu zote zitakamilishwa. Alitoa wito kwa wananchi wote ambao uhakiki wao umekamilika kuendelea kuamini serikali yao kwa kuwa ni serikali sikivu na inayotekeleza ahadi zake.

Akizungumza katika tukio hilo, Mhe. Kalima alimpongeza Mkuu wa Mkoa kwa kuahirisha ratiba zake ili kufika Mkinga kushirikiana na wananchi katika hatua muhimu ya utekelezaji wa mradi wa kitaifa.

“Kwetu sisi Mkinga tunajivunia uwepo wako, Mhe. Mkuu wa Mkoa. Kama ambavyo tumeona kupitia hotuba za viongozi waliotangulia, wananchi wamekupa imani kubwa na tunashukuru kwa namna unavyosimamia masuala ya maendeleo,” alisema.

Katika hatua nyingine, Mhe. Kalima alitangaza kuanza kwa ziara maalum ndani ya Kata ya Mwakijembe wiki ijayo, ziara itakayompa nafasi ya kusikiliza moja kwa moja kero za wananchi katika kila kijiji na kufanya maamuzi ya haraka ya kukabiliana na changamoto zinazoibuliwa.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA October 16, 2023
  • HATI MILIKI ZA ARDHI ZILIZOKAMILIKA WILAYA MKINGA December 04, 2022
  • KUSAFISHA MAENEO KWA WAMILIKI WA VIWANJA MKINGA August 12, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA July 18, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA CHAKULA DUNIANI KWA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA UZALISHAJI WA CHAKULA

    October 16, 2025
  • TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA CHAKULA DUNIANI KWA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA UZALISHAJI WA CHAKULA

    October 16, 2025
  • WITO WATOLEWA KWA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA KWA AMANI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29,2025

    October 23, 2025
  • MAKARANI WAOMNGOZAJI WAPIGA KURA WAASWA KUWA WAADILIFU

    October 25, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

Angalia zaidi

Kurasa za Haraka

  • Fomu za Maombi
  • Habari

Kurasa Mashuhuri

  • OR- TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Salary slip portal
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Taifa
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Kasera, Tanga -HorohoroRoad

    Postal Address: P O Box 6005 Tanga

    Simu: +255 027-2660501

    Simu: +255 684 625 299

    Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Huduma

Mkinga dc @ 2017