• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mkinga District Council
Mkinga District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Livestock and Fishary
      • Works and Fire Recure
      • Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ugavi
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Legal
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma wa Maji
    • Huduma ya Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Maktaba ya Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Matukio
    • Habari
    • Matukio

MHE. MWAKIOJA AWASISITIZA WANANCHI KUENDELEA KUIAMINI SERIKALI

Posted on: December 5th, 2025

MHE. MWAKIOJA AWASISITIZA WANANCHI KUENDELEA KUIAMINI SERIKALI

Na: Nassoro Rashid - Mkinga

Mbunge wa Jimbo la Mkinga, Mhe. Twaha Said Mwakioja, amewahakikishia wananchi wa Kata ya Mwakijembe kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kusimamia haki na ustawi wa kila mmoja, huku akiomba wananchi waendelee kuwa na imani na serikali wakati taratibu za kutatua changamoto zao zikiendelea kufanyiwa kazi.

Mwakioja alitoa kauli hiyo Desemba 04, 2025 wakati akishiriki hafla ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Buriani, ya kukabidhi hundi za fidia kwa wananchi waliohamishwa kupisha Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi katika Kijiji cha Mkota, Kata ya Mwakijembe, Wilaya ya Mkinga.

Mbunge huyo alibainisha kuwa changamoto za wananchi ni mchakato unaohitaji ushirikiano wa pande zote, na akatoa ahadi ya kufanya ziara kijiji kwa kijiji ili kusikiliza kero na kuzifikisha katika mamlaka husika kwa utatuzi wa haraka.

Aidha, Mhe. Mwakioja alitumia nafasi hiyo kuwasilisha maombi mawili muhimu kwa Mkuu wa Mkoa kwa niaba ya wananchi:

Kwanza, kuwatupia jicho la huruma wananchi 25 ambao hawajapata stahiki zao za fidia kutokana na changamoto za kinyaraka.

“Nafahamu Mhe. RC ni mtu mwenye huruma na anayetekeleza maelekezo ya Rais wetu. Naomba wananchi hawa 25 wapewe kipaumbele ili nao wapate haki yao. Tumeona hata watumishi waliowahi kuachishwa kutokana na vyeti feki walilipwa stahiki zao kwa maelekezo ya huruma ya Mhe. Rais. Naamini na hili litawezekana,” alisisitiza.

Pili, aliiomba Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kufuatilia kwa karibu eneo jipya walilopelekwa wananchi hao ili kuhakikisha lina miundombinu ya msingi ikiwemo maji, barabara na mazingira rafiki kwa makazi.

“Tuelekeze nguvu kuhakikisha eneo hili si tengefu tu kwa jina, bali ni mahali panapoweza kuwawezesha wananchi kuishi kwa furaha, amani na tabasamu usoni,” alisema.

Katika hatua nyingine Mhe. Mwakioja aliwashukuru Wananchi kwa namna walivyotekeleza vyema zoezi la uchaguzi mkuu uliopita na kuonesha imani kubwa kwa Serikali kwa kumpa kura nyingi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan; Mbunge wa Jimbo hilo; na Diwani wa Kata ya Mwakijembe, Mzee Mwadika.

“Nawashukuru sana ndugu zangu wa Mwakijembe. Pamoja na changamoto zenu nyingi, mmeendelea kuiamini Serikali yetu. Mmetupa kura za kishindo na kutuonesha dhamira yenu ya kutuunga mkono. Tutaendelea kuwa nanyi na kusikiliza kero zenu,” alisema.

Aidha alimuomba Mkuu wa Mkoa kutoa nafasi fupi kwa Diwani wa Kata hiyo, Mzee Mwadika, ili kuwahutubia wananchi wake kama ishara ya umoja na mshikamano katika hatua za kutatua changamoto zilizopo.

Tukio hilo limeacha matumaini makubwa kwa wananchi wa Mwakijembe, huku Serikali ikisisitiza kuwa hakuna mwananchi atakayeachwa nyuma katika kuhakikisha haki, fidia halali na ustawi wa jamii unaimarishwa.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA October 16, 2023
  • HATI MILIKI ZA ARDHI ZILIZOKAMILIKA WILAYA MKINGA December 04, 2022
  • KUSAFISHA MAENEO KWA WAMILIKI WA VIWANJA MKINGA August 12, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA July 18, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA CHAKULA DUNIANI KWA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA UZALISHAJI WA CHAKULA

    October 16, 2025
  • TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA CHAKULA DUNIANI KWA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA UZALISHAJI WA CHAKULA

    October 16, 2025
  • WITO WATOLEWA KWA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA KWA AMANI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29,2025

    October 23, 2025
  • MAKARANI WAOMNGOZAJI WAPIGA KURA WAASWA KUWA WAADILIFU

    October 25, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

Angalia zaidi

Kurasa za Haraka

  • Fomu za Maombi
  • Habari

Kurasa Mashuhuri

  • OR- TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Salary slip portal
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Taifa
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Kasera, Tanga -HorohoroRoad

    Postal Address: P O Box 6005 Tanga

    Simu: +255 027-2660501

    Simu: +255 684 625 299

    Barua Pepe: Info@mkingadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Huduma

Mkinga dc @ 2017